Friday, February 19, 2010

Kamata! Shika! na mwenyewe nyuma…..!

Na Deus Bugaywa

Ukiwaangalia Watanzania wa leo utaona kwenye fikra zao, nyuso zao na hisia zao utaona wazi kabisa kuwa iko kiu ya mabdiliko. Watu wanataka mabadiliko wamechoka na mazoea waliokuwa nayo na ambayo yanaendelea kuwafanya wawe dhalili.
Kila mtu anatamani mambo yaache kuwa na hali ilivyo sasa, anatamani yachukue mkondo mpya na njia mbadala ambayo inaweza kuwa na matumaini. Katika hali hii unatarajia kuwa wao ndiyo wawe chemichemi na chachu ya mbadiliko.
Bahati mbaya kwetu ni kwamba, tunataka na kutamani mabadiliko lakini hatuko tayari kulipa gharama za mabadiliko hayo. Tunataka matokeo yaje tu kutoka hewani bila sisi kuhusika kwa namna yeyote ile kuyasababisha.
Katika hili tunapaswa kujifunza kwa ujumbe wa mabadiliko wa Rais wa Marekani Barack Obama kwamba “The change we seek will not come easy, that it will not come without its share of sacrifice and struggle”, kwamba mabadiliko tunayoyataka hayawezi kuja kirahisi na hayawezi kuja bila juhudi na kujitolea.
Majitoleo yanayozungimziwa hapa ni pamoja na kukubali kuachana na mazoea mabaya ambayo tunayaona kuwa kama sehemu ya maisha yetu, kwamba hata kama tunaumizwa sana na mazoea hayo, hatuko tayari kuyavua na kuvumilia uchungu kidogo wa muda ili tupate nafanikio ya muda mrefu.
Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi ambao Watanzania tunatakiwa kutumia haki yetu ya kikatiba kuchagua aina ya viongozi ambao wanaweza kutuletea mabadiliko tunayoyatamani. Tunatakiwa tuutambue ukweli kwamba mambo mazuri ya kimaendeleo tunayoyatamani yana uhusiano wa moja kwa moja na aina ya viongozi tunaowachagua.
Jiulize Mtanzania, wewe mahali ulipo una mwakilishi wako mbunge na diwani, lakini kuna kero nyingi sana mtaani kwako, katani na jimboni kwako, kiongozi huyo anatakiwa kuwa mhamasishaji wa maendeleo katika jimbo na kata yenu.
Yako mambo ambayo hayahitaji hata nguvu ya serikali kuyafanya yawezekane, mambo mengine kama barabara za jimboni kwenu, huduma za maji na vitu vya aina hiyo vinategemea sana aina ya kiongozi wenu, kama ana sifa za kufaa kuwa kiongozi anaweza kabisa kuwahamasisha ninyi wanajimbo na kata na kuishwishi serikali kuweka nguvu kidogo ili kufanikisha maendeleo yenu.
Wako Watanzania leo wana mbunge huyo huyo kwa miaka 15 au zaidi lakini hajawahi kuwa na mchango wa maana kwa katika kuhamasisha maendeleo ya jimbo lake, huyu hata kama ni mjombe wenu, mmezalia kijiji kimoja au ni swahiba wako sana, hafai kuwa mbunge wa jimbo lako.
Kama katika miaka hiyo kwa vipindi vitatu hajafanya mambo ya msingi, anaonekana jimbo mara moja kwa miezi sita, kwa mwaka anaonekana jimboni mara mbili kama sikuku za Eid el fitri na Eid al Haji, huyu hata akipewa miaka 25 mingine hawezi kuleta mabadiliko ya maana jimboni kwako.
Wabunge wa aina hii ni wajanja sana katika kipindi kama hiki anakuwa mnyenyekevu na vizawadi kwa viongozi mbali mbali wa chama na watu wenye ushawishi jimboni ili waweze kurubuni ninyi mliobaki ili mmuone ni aina ya mtu kweli mnayemhitaji.
Huyu katika hali ya kawaida anacheza na akili zenu tena ni kashfa kwenu ninyi kwa kuwa anaowaona kama watoto wadogo mnaoweza kudanganywa na ‘peremende’ mkadanganyika, na anakuwa anawapuuza hivyo hivyo kila mwaka ndiyo maana bado ni mwakilishi wenu kwa miaka yote hiyo.
Wanaharakati wa ukombozi wanamsemo mmoja kuwa “The most potent weapon of the oppressor is the mind of the oppressed”, kwamba silaha muhimu sana kwa wakandamizaji ni akili za waandamizwaji.
Ni kweli wala hatuwezi kubishana katika hili, kwamba viongozi wetu hawa wanaotuongoza wanatunyanyasa na kutumia nafasi za umma tulizowapa dhamana kutuongoza kuelekea kwenye maendeleo yetu kama taifa, wanazitumia kwa manufaa binafsi kwa sababu ya umbumbu wetu.
Mnamwona mbunge wenu yuko ‘bize’ na mambo yake kuliko ya umma ambayo aliomba kuwa mtumishi wenu ili awatumikie, badala yake hata kumona tu mmweleze maoni yenu na jinsi mnavyoona mnaweza kukabiliana na changamoto zenu katika jimbo inakuwa ni kazi ngumu kumuona kama vile unataka kuonana na malkia.
Msomaji mmoja wa Kanda ya Ziwa alieleza masikitioko yake jinsi ambavyo wamefanya juhudi za kutaka kumuona mbunge wao kwa muda wa mwaka mzima lakini hawakufanikiwa badala wanaishiakuelekezwa kuonana na katibu wake.
“Hata tulipompigia simu mara kadhaa, kwa sababu hata jimboni haishi, alituelekeza tuonane ana katibu wake tu, tukaisisitiza katibu anajua na hana msaada akasema akija atatupatia nafasi tumuone, siku amekuja kulikuwa na mafuriko ya watu hatukumuona mpaka tukakata tama, sasa ndugu mwandishi huyu kweli anafaa kuwa kiongozi?”, alihitimisha msomaji wangu kwa kunihoji.
Nilimwelewa mahangaiko aliyokuwa nayo pamoja na wananchi wenzake, lakini nilimjibu nikamwambia, katika kila jamii kuna uwezekano mkubwa wa kupata kiongozi anayewastahili zaidi kuliko mnayemtaka, kwa hiyo kumlaumu Mheshimiwa huyo inaweza kuwa ni kumonea kwa kuwa wakati wananmchagua hawakugalia sifa za mtu wanayemchagua na kuwianisha na changamoto zao ili kujua kama anaweza kuwa ni aina ya kiongozi wanayemhitaji.
Kwamba huenda walimchagua kwa kuwa ni mtu maarufu jimboni kwao, au ni tajiri sana, au ni ndugu yao, au aliwahonga sana kuliko wagombea wenzake, au alikuwa anapigiwa kampeni na watu wanaowaheshimu sana humo jimboni, nikamweleza hizo zote na zingine za kufafana nazo siyo sifa na wala hazitakaa ziwe sifa za kiongozi bora.
Na hicho ndicho huwa tunakifanya Watanzania tunapoingia katika vyumba vya kupigia kura, iwe katika uchaguzi wa kura za maoni au uchaguzi mkuu, tunatumia vigezo vya ajabu sana na kwa kweli, ashakum si matusi, ni vya kipumbavu kuchagua viongozi wetu.
Mwaka huu kama kweli ile kiu ya mabadiliko iliyopo ni ya kweli, kama sio unafiki, basi ni lazima Watanzania katika ngazi zote bila kujali kiwango cha elimu ya mtu, aina ya kazi unayofanya au mahali unapoishi, tubadilike kwanza sisi wenyewe na tuwe tayari kulipa gharama za mabadiliko.
Hivi kuna haja gani ya kuwa na mbunge kwa miaka 10 au zaidi lakini ambaye hana mchango wowote wa maana kwa maendeleo ya jimbo, naomba nieleweke ninaposema maendeleo ya jimbo, sizungumzii vijizawadi na vitakrima vinavyotolewa kwa viongozi wenu wa matawi au kata, au hata kwa baadhi ya watu maarufu, ambavyo mimi ninaviita ni vijirushwa katika ngozi ya zawadi.
Maendeleo ninayozungumzia hapa ni ya jumla na yanayofaidisha jamii nzima kama maji, barabara, elimu na huduma zingine za jamii ambazo kila mwanajimbo anaweza kujivunia kuwa hakupoteza kura yake bure.
Na kuleta mchango katika hili siyo lazima mtu awe na pesa za kutoa mfukoni, kwanza mtu mwenye kutoa pesa mfukoni kwa ajili ya maendeleo ya jimbo, huyo hafai na hana sifa za kuwa kiongozi, mchango ninaouzungumzia mimi hapa ni jinsi anavyowaunganisha wanajimbo kuweza kuzikabili changamoto zenu kwa kutumia rasilimali chache mlizonazo ili kuweza kujikwamua na hali mliyomo na kupiga hatua.
Chonde chonde Watanzania, mwaka huu ni wa ukombozi, tusipige kura kwa mazoea, tuchague aina ya mtu ambaye tunaamini anaweza kuwa msaada kwetu na siyo kwa kuwa eti ni tajiri sana, tukubali kuwa chanzo cha mabadiliko tunayoyatamani. Unapopiga yowe la Kamata mwizi! Kamata mwizi! ni sharti na wewe uwe nyuma ukimfukuza mwizi huyu kwa juhudi kubwa, ndipo wengine watakuunga Mkono.
Kadhalika mabadiliko na ukombozi wa kweli wa nchi hii unahitaji mapinduzi ya kweli, siyo ya mtutu wa bunduki wala mapanga, bali kwa sanduku la kura, ambayo lakini yatatokana na kubadilika kwa mtazamo wetu wakati wa kupiga kura.
Mungu ibariki Tanzania
drbugaywa@yahoo.com, 0754 449 421

Friday, February 5, 2010

CCM, mchelea mwana kulia…!

Na Deus Bugaywa



Chama Cha Mapinduzi leo kinatimiza miaka 33 tangu kuzaliwa kwake tarehe 5, Februari, 1977 baada ya kuungana kwa vya vya TANU na ASP na kuunda chama kimoja kilichoitwa cha Mapinduzi.

Kiliunda cham kipya kikiwa ni mrithi wa wazazi wake waliokitangulia ambao kwa namna moja ama nyingine walihusika na ukombozi wa Tanzania na kutuwezesha kupata uhuru toka wa Mkoloni na Usultani wa kiarabu kwa Zanzibar.

Hiki ni chama ambacho kiliundwa kwa makusudi maalum ya kuwatetea wakulima na wafanyakazi wa Tanzania , kilikuwa na malengo mahsusi ya kumkomboa mwananchi mnyinge kutoka katika unyonge wake na kumfanya mtu anayetahamniwa.

Kwa sababu madhumuni ya kupigania uhuru hayakuwa kumwondoa tu mkoloni wa kizungu ndio unyonge wa mwafrika wa Kitanzania utakuwa umekwisha, ndio maana kikaundwa chama hiki ili kumwezesha mwananchi huyo kupata na kuweza kuiishi tafsiri na maana halisi ya kuwa uhuru.

Kwa maana nyingine CCM kiliundwa ili kiweze kumwzesha Mtanzania kujikinga na wimbi la wanyonyaji na walanguzi wa wakati huo ambao waliona na kamiani kwamba mafanikio yao hayawezi kuja bila kuwafanya watu wengine kuwa dhalili.

Kwa hiyo siyo bahati mbaya kwamba moja ya misingi iliyokiundiwa chama hiki iliyolithiwa toka TANU ni msingi wake wa kwanza unaowataka wanachama wake kuamini kwa dhati kwamba binadmau wote ni sawa na ndugu zangu na Afrika ni moja.

Tena ikasisitizwa kwamba pale mtu anapopewa heshima ya kuwangoza au kuwatumikia Watanzania wenzake asijione kuwa ndiyo amekuwa ‘mkoloni mweusi’ wa kuwanyasa wenzake au kutumia mali ya umma kama vile ni mali yake binafsi.

Hawa wakakukbushwa kuwa cheo ni dhamana na wakatakiwa kutotumia vyeo hivyo kwa manufaa yao binfasi isipokuwa kwa ajili ya utumishi na maslahi ya umma na ni umma tu ndio unaotakiwa ufaidike na utumishi wa mtumishi huyu wa umma na vinginevyo.

Bila shaka tutkubaliana kwamba msingi mwingine muhimu katika ukuaji na hatimaye kufikiwa malengo ya taasisi au chama chochote kile ni ukweli, kwa maana na tasira zake zote, wana CCM hapa walisisitizwa kusema kweli daima na fitina kwao iwe mwiko.

Hii na Minsingi mingine imekifanya chama hiki leo kufikia umri huu na kukifanya moja vyama vikongwe kabisa vya siasa sio tu katika Tanzania lakini pia ndani ya bara la Afrika.

Bila shaka wana CCM wanahitaji pongezi hili, kufikia umri huu ni kazi kubwa mabyo siyo vyama vingi vyenye lika moja an CCM vimeweza kufikisha umri huo vikiwa bado ni vyama tawala. Kwa hili tu wanastahili pongezi hata kama namna ya kufikisha kwao umri huu kunahitaji mjadala lakini walau wafika.

Pamoja na pongezi hizo, hata hivyo, ni jambo jema pia kwa wenye chama chao hiki, kuongozwa na hekima ya kawaida kabisa katika maisha haya kwamba, kitu cha muhimu katika maisha haya siku zote siyo pale ulipo isipokuwa ni wapi nuanelekea.

Mtu yeyote makini habweteki na kufika pale alipofika, isipokuwa anakaza mwendo kuweza kuongeza nguvu na kurekebishwa mwelekeo wake ili asiende kombo. Atatumia uzoefu, kwa kutahimini uwezo na mapungufu aliyokuwa nayo katika kufika hapo alipofika.

Ndio maana ni muhimu kwa wanachama wa chama hiki wanapofurahia siku ya kuazaliwa kwa chama chao, wajiulize swali wana umbali gani wa kwenda wakiwa katika furaha hii ya sasa?

Watakubaliana na mi kwamba wamefika hapa kutokana na misingi imara iliyosimamiwa na uongozi thabiti wa chama hicho, ambao sina hakika sana kama wanaweza wakasimama kifua mbele wakasema wanao uongozi wa aina hiyo ndani ya chama chao kwa sasa unaweza hata kushabihiana kwa nusu wa ule uliowaasisi na kuwawezesha kuweza kusafiri safari hii ndefu mpaka hapa walipo leo.

Wenyewe ni mashahidi wa jinsi ambavyo mpaka hapa walipofika bado wanasafiria kivuli cha utahbiti wa viongozi waasisi wao hata baada ya miongo miwili kupita tangu kiazi chao kipya kiakbiziwe chama.

Alichofanikiwa kwa kiasi kikubwa ni kuivunja vunja miiko hiyo n badala yake sasa chama kimekosa ile maana yake halisi ya kuwa kundi la watu wenye dhamira na nia moja katika kutekeleza malengo yanayofanana.

Leo katika CCM wapo wanachama mahiri wengi tu lakini, kama si mnafiki huwezi kukiita chama hicho ni kimoja kwa hali ilivyo sasa. Ni kundi moja ambalo lakini kila mwana kikundi anasababu zake tofauti kabisa na mwenzake za kuwemo ndai ya kundi hilo na namna tofauti kabisa tena zinazokinzana za kueteleza malengo hayo.

Ni kama timu inayoundwa na wachezaji wazurina mahili wa kimataifa lakini ambao hawana ushirikiano wa kitimu ‘team work’. Kila mchezaji anakuwepo pale isyo kwa ajili ya kufunga magoli lakini kwa ajili ya kuonyesha jinsi alivyo mtaalam kulamba chenga maadui zake, na kuwaonyesha maadui zake (wa ndani na nje ya timu) namna anavyoweza kumudu mpira, lakini ujuzi huo haumsaidii kufunga magoli.

Ndiyo umvyoweza kuiliezea CCM ya sasa, ambayo pamoja na kusherekea umri huo uliotukuka ukilinganisha na vyama vingine vya siasa nchini, kwa hakika badao kinaoneka kana kilizaliwa baada ya mfumo wa vyama vingi, na kwamba labda ndio kinajifunza siasa. Ukikitazama kwa makini kwa kweli huwezi ukaona umri wake unaakisiwa katika namna kinavyojiedesha.

Kwanini kimefika hapa, bila shaka ni kutokana na kutosikia la mkuu na hivyo kinajikuta taratibu na kwa uhakika kinapoteza miguu. Wahenga wetu wamewahi kutuonya kuwa ‘Mchelea Mwana kulia, hulia yeye’.

Kwamba ukiwa wewe ni mlezi wa mtoto halafu anapofanya kosa hutaki kumkanya kwa vile unaogopa atalia basi wewe ndiyo ujiandae kulia. Na hiki ndicho kilichoikuta CCM.

Kumekuwa na ungonjwa mbaya kabisa usiofaa wa kulindana ndani ya chama hiki, mtu akifanya kosa ambalo kwa tartaibu za kawaida tu ama anatakiwa awajibike au kama si muungwana anakuwa na kiburi hataki kuwajibika basi awajibishwe na mamlaka anayowajibika kwayo.

Hili limekuwa haliwezekani ndani ya chama, kiemfika mahali kinadhani kwamba ni chenyewe tu chenye hati miliki ya kutawala nchi hii, na zaizi sana kinadhani Watanzania wote ni wajinga kiasi kwamba wanaweza kuafanya madudu yao halafu wakaendelea kuaminika tu na wananchi kwa kiwango kile kile, hili ni kosa moja kubwa wanalofanya CCM.

Kiongozi wa chama anapokosea au anapopatikana na kashfa ambazo zinaweza kuharibu sifa na jina la chama kwa wananchi utasikia viongozi wa cham tena wengine wa kitaifa eti wakikitetea chama kwamba huyu aliyefanya hivyo mwanachama wa CCM siyo CCM.

Halafu mtu huyu hata hawajiishwi walau kisiasa ili kweli chama kiwezi kujitenga nae na wananchi wajue kweli kwamba kimejitenga na mkosaji au mtuhumiwa huyo, lakini kuendelea kumkana mtuhumiwa halafu upande wa pili kinaendelea kumkumbatia, huko ni kujiandalia mauti.

Ni vyema, kama inataka kuendelea kuishi, CCM ikajifunza kwa wazee wenzake Kenya , Zambia , Malawi ili irekebishe makosa yake. Kila lakheri CCM katika umri huu

drbugaywa@yahoo.com 0754 449 421

Uharamia Ziwa Victoria na hatma yetu

Na Deus Bugaywa



Historia au uzoefu, ilisemwa, ni mwalimu mzuri sana hasa kwa wanafunzi makini na wanaothamini maana ya kujifunza. Kwa kuwa kila kinachotokea katika maisha yao kiwe kibaya au kizuri kinakuwa ni somo murua ambalo linawafanya ama waweke mbinu za kukiendeleza chema hicho au mikakati ya kuakabiliana na kukomesha chochote kibaya kilichotokea.

Inawezekana sisi, Tanzania , bahati hii ya kuwa wanafunzi makini wa uzoefu na historia imetupita kushoto na kwa hiyo tunaishi tu ili mradi kunakucha na maisha yanaendelea ama kwa wema au ubaya, potelea mabali Mungu ndiye ajuaye.

Pengine sisi ni mfano halisi wa jamii zile zinazoongozwa na msemo ya wahenga wetu kwamba kwenye miti hapa wajenzi, kuna wafunga fito tu. Nazungumzia juu ya usimamizi wa rasilimali zetu na jinsi mabayo zinaweza kutuletea anufaa yanayoshabihiana kweli na umiliki wetu wa rasilimali hizo.

Jinsi mabavyo rasilimali hizi zinaweza kunufaisha mwananchi Mtanzania mwenye bidii ya kazi ambaye ameamua kutumia rasilimali ambazo taifa hililimejaliwa kuwa nazo kuyafanya maisha yake yawe ya kiutu, heshima na hadhi ya binadamu anayeheshimika na kuthaminiwa.

Moja ya tunu ambazo Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema, ametujalia ni pamoja na kuwa wamiliki wa sehemu zaidi ya nusu ya Ziwa kubwa kuliko yote katika Afrika na la pili kwa Ukubwa duniani baada ya Ziwa Superior liliko Kaskazini mwa Amerika, ninazungumzia Ziwa Victoria .

Ziwa hili lenye ukubwa wa kilomota za mraba zipatazo 68, 800 limetuunganisha na nchi mbili za Afrika Mashariki za Kenya na Uganda kwa uwiano wa umiliki wa Tanzania asilimia 51, Uganda asilimia 43 na Kenya asilimia 6.

Licha ya kuwa Ziwa hili ni chanzo muhimu cha maji kwa wakazi wanaoishi ndani ya bonde la Ziwa Victoria, pia ni chanzo muhimu cha malighafi za viwada vya samaki na mazao yake, kilimo cha umwagiliaji, uvuvi na shughuli nyingine nyingi, zinazolifanya Ziwa hili kuwa tumaini la maisha kwa watu wapatao milioni 30 wanaoishi katika bonde lake, bado hali ya usalama wa watu na mali zao siyo nzuri.

Hali ya usalama ndani ya Ziwa hili linabaki kuwa changamoto kubwa kwa serikali, jeshi la polisi na wananchi kwa ujumla kwa kuwa hakuna anayeweza kusema hahusiki moja kwa moja na hali ya kukosekana kwa usalama ndani ya Ziwa hili.

Mazingira na miundombinu ya visiwa vingi vilivyoko ndani ya ziwa, vikiwemo vyenye makazi ya kudumu na vingine vinavyokaliwa na wavuvi kwa misimu kama kambi za uvuvi ni moja ya changamoto kubwa katika kuhakikisha usalama ndani ya ziwa hili.

Utete wa usalama unachangiwa pia na kuwa na mipaka inayotenganisha nchi zetu tatu ndani ya Ziwa ambako wakati mwingine, bila ushirikiano wa dhati kutoka kwa nchi zote zinazougana ndani ya ziwa katika kuimarisha ulinzi, udhibiti wa uharamia linakuwa ni suala gumu sana .

Si hivyo tu upana wake pia na dhana duni za askari wetu hasa katika kukabiliana na uhalifu kwenye mazingira kama hayo ya majini nayo ni moja ya chanagmoto kubwa sana .

Urefu wa Ziwa hili toka Kaskazini hadi Kusini ni kilomita 337 na upana wake toka Mashariki mpaka Magharibi ni kilomita 240, katika hali ya upana wa namna hii na kuwepo kwa visiwa vingi na ambavyo ni vituo muhimu kwa shughuli za uvuvi na uduni wa vyombo vya doria ndani ya ziwa vinalifanya kuwa sehemu salama sana kwa wezi na maharamia.

Itakubukwa kwamba upo wakati, kuna baadhi ya watu wenye pesa ambao walijitangazia ‘vijamhuri’ vyao kwenye baadhi ya visiwa, wao ndio wakawa ‘serikali’ za visiwa hivyo. Serikali mkoa wa Mwanza ilikanusha sana habari hizi, ingawa hili halikuondoa ukweli.

Watu hawa, wenye pesa na mtandao mpana, walikuwa wanaendesha visiwa hivyo na kuwafanya wavuvi kama mali yao , kwa kuwa ndani ya visiwa hivyo kwa mujibu wao ‘hakuna serikali’.

Vitendo vya kikatili na kinyama ndani ya ziwa hili kweli vingeweza kukusadikisha kweli kwamba serikali haipo huko. Kuvamiwa kwa wavuvi na kuzamishwa majini huku majambazi hao wakijichukulia kila kitu, ulikuwa ni utaratibu wa kawaida, Kulikuwa na mtandao mkubwa ambao ulikuwa na kazi ya kuiba mitumbwi ya injini ambao ulikuwa na matawi yake mpaka Kigoma, hapa jeshi la polisi lilifaniwa walau kuuyumbisha mtandao huu kwa kuwakamata baadhi ya wahusika hali ikawa shwari kidogo, sina hakika kaa umekufa.

Uko mtindo uliokuwa maarufu sana ziwani humu, ambao unaitwa ‘Car wash’ au ‘kaptula’, hii ilikuwa inamaanisha maharamia wanapowavamia wavuvi wanawataka ama wachague kukatwa mikono na mabega (car wash) au miguu (kaptula). Hapa napo wavuvi waliteseka vya kutosha.

Ninachokikusudia hapa ni kueleza ukweli kwamba hali ya usalama katika ziwa hili ni tete sana na halijawahi kuwa salama isipokuwa ukatili na unyama huu unabadili sura tu.

Tukio la hivi majuzi katika Kisiwa cha Izinga lilipoteza maisha ya Watanzania 13 na kujeruhi wengine 17 ni ya aina nyingine tu ya jinsi ukatili katika ziwa hili unaweza kuvaa sura mbali mbali.

Kinachotakiwa ni kuweka mikakati ambayo itasaidia kuhakikisha usalama wa watu na mali zao ndani ziwa hili na kulifanya kuwa ukanda muhimu wa uzalishaji mali kwa ustawi wa watu wetu na taifa letu kwa ujumla na siyo kualichia taratibu kugeuka kuwa kaburini na chanzo cha umaskini, ulemavu na mauti kwa Watanzania.

Ni kweli kwamba Operesheni maalum kama hii inayoendeshwa sasa ndani ya Ziwa hilo na Kamanda Tossi iliyopewa jina la ‘Operesheni Chakaza’ ni muhimu kwa ajili ya kutuliza hali ya mambo na kuwakamata watuhumiwa wa mauaji ili wafikishwe mbele ya mkono wa sheria.

Pamoja na umhimu huo, operesheni hizi haziwezi kwa zenyewe tu kurejesha hali ya utulivu na usalama ambao watu wanauhitaji kwa ajili ya kujiletea maendeleo kwa shughuli za uvuvi na zingine zinazofanyika ziwani humo na kwenye visiwa vyake.

Wananchi pia wanatakiwa kuwa ndio walinzi namba moja wa maslahi yao , kwa kutoa ushrikiano kwa vyombo vya ulinzi, kwa kutoa taarifa kwa watu wanaowahisi wana nyendo zinazoashiria mashaka.

Kwa kuwa ni lazima pia tukiri kwamba kama jinsi miundo mbinu ya ziwa na visiwa hivyo ilivyo na ugumu katika kuimarisha ulinzi wa Ziwa hilo ndivyo pia ilivyo vigumu kwa maharamia kukamilisha mipango yao ya uhalifu, wanafanikiwa kwa kuwa wanapewa ushirikiano na rai wenyeji wasio wema.

Tukiacha kushirikiana nao, na tukiamua kuwadhibiti hawa wachache wanaoshirikiana na majambazi hawa, tunaweza kabisa kudhibiti hali ya usalama wetu bila gharama kuwa na ugumu usiokuwa wa lazima.

Bila kuchukua hatua hizi, tutaendelea kuzifanya rasilimali zetu kama iliyo kwenye madini, kuwa vyanzo vya laana na mauti badala ya kuwa neema kwa hatma ya Tanzania ya leo na ijayo.

Mungu ibariki Tanzania

0754 449 421 drbugaywa@yahoo.com

Ukombozi Tanzania uko mikononi mwako

Na Deus Bugaywa



Ni kweli kwamba maendeleo katika sehemu yeyote duniani yanaletwa na watu wenyewe, kwamba hakuna muujiza unaoweza kujitokeza kumletea mtu maendeleo isipokuwa kwa kufanyakazi kwa bidii na maarifa.

Lakini katika Afrika na Tanzania ukiwa mmoja wa mifano halisi imedhirika sasa kwamba viongozi wana mchango mkubwa sana katika kuwa chanzo cha matatizo na umaskini mkubwa kwa watu wake.

Umaskini na matatizo ya taifa na wananchi unatokomezwa kwa mipango na mikakati mahsusi inayopangwa na kutekelezwa kwa makini na viongozi shupavu na wenye uzalendo wa kweli kwa taifa lao.

Viongozi wa aina hii ni wale tunaowaita viongozi watumishi, ni aina ya viongozi ambao wanajua wao ni watumishi tu wa umma wa jamii wanayoingoza, na hivyo wanaheshimu na kuthamini dhamana walizopewa na watu wao.

Katika nchi zetu hizi uongozi ni suala tete sana , ni mchanganyiko wa watu wa aina mbali mbali ambao wengine hata hawana hata chembe ya sifa ya kuitwa viongozi. Ni ndoto ya kila mwananchi kuwa na viongozi bora ambao hawa wanaweza kuleta matumaini kwa watu wao, ya kulirejesha taifa katika njia ambayo inaweza kusaidia kulikwamua taifa kuondokana na umaskini uliopindukia.

Kwa upande mwingine wapo viongozi wabovu ambao kwa uongozi ni njia ya makato kufikia enzi na heshima ya utukufu wa utajiri kwa njia ambazo siyo halali. Kwao kutumia kila aina ya hila na mbinu chafu kujinufaisha kwa gharama za umaskini wa wananchi waliowapa dhamana hizo.

Wananchi wengi kwa sasa wanajua wazi na kwa uhakika jinsi ambavyo viongozi wanapuuza sauti zao dhidi ya rushwa, wanajua jinsi vingozi waivyowageuza ngazi za kupandia kuuendea ufalme wa ukwasi mkubwa katikati ya lindi kubwa la umaskini.

Kama tunakubalina kimsingi kwamba kuendela au kutoendelea kwa taifa kunategemea kwa kiasi kikubwa sera na mipango taifa iliyojiwekea na upeo wa viongozi wake waliopewa jukumu la usimamizi wa rasilimali za taifa.

Tukiwa tunaelekea katika uchaguzi mkuu baadae Mwezi oktoba mwaka huu, ni lazima kama wananchi wa taifa hili tukae na kufanya tafakuri makini juu ya hatma ya taifa letu.

Uko ukweli wa hakika kwamba fikra, tabia na mienendo na mazoea yaliyotuingiza katika matatizo tuliyo nayo kwa sasa kama taifa, hasa ya usimamizi mbaya kabisa wa rasilimali zetu hayawezi kutusaudia kuyatatua matatizo haya, kwa kifupi ni kwamba mfumo uliotuingiza katika matatizo haya hauwezi kututoa katika matatizo hayo.

Tunahitaji mfumo mpya na fikra za kimapinduzi ili kuweza kutumia vyema fursa ya kuweka viongozi katika madaraka, ni lazima historia itufundishe na kama tusipokubali kuwa wanafunzi wazuri wa historia yetu wenyewe, hatutakuwa na budi ila kuvunjika guu.

Watanzania tumekuwa na tabia ya kufanya chaguzi zetu kwa mazoea tu bila kuwa na agenda mahsusi na kujiuliza swali ya msingi ya kwanini tunafanya uchaguzi. Tunauona kila uchaguzi kama ni tukio la kawaida tu ambalo linakuja na kupita kama yanavyokuja matukio mengine yote.

Lakini ni vyema mwaka huu tukaamua kubadilika, kw amantiki kwamba mpaka tutakapobadilika sisi wenyewe waannchi mmoja mmoja, hatuwezi kutarajia mabadiliko kutoka kwa viongozi wetu.

Ni kweli kwamba baadhi ya viongozi hawa wamekuwa ndio chanzo cha matatizo yetu, kwa kukosa kwao umakini, kutingia katika mikataba isiyo na maslahi kwa taifa, kuendekeza rushwa na ufisadi, na kutothamini dhamana zao na wakati mwignine uwezo mdogo wa kuongoza.

Abraham Lincoln alipoitafsiri Demokrasia kuwa Serikali ya watu, inayotokana na watu kwa ajili watu hao hao, hakuwa na maana nyignine isipokuwa watu wachague viongozi ambao watukuwa wanaendesha serikali wa matakwa na amslahi ya watu wenye taifa husika waliowachagua viongozi hao.

Kwa hiyo uchaguzi kwa maana nyingine ndio njia pekee anaypata fursa mwananchi kuamua serikali yake iendeshweje na nani aiendeshe serikali hiyo. Hapa kura inakuwa na ngvu na mamlaka makubwa kuliko bunduki au kombora lolote lile.

Bahati yetu mbaya ni kwamba wananchi wengi hatujajuwa au sijui ni kwa kusudi tu, tunaamua kutumia kura zetu kama karata za kuchezea kamari, halafu baada ya uchaguzi au kiongozi akishakuwa tayrai kwenye hatamu za uongozi tunamuogopa anatuburuza anavyotaka na kujichotea rasilimali zetu kama zisizokuwa na mwenyewe halafu tunabaki tunalalamika na kunung’unika kana kwamba hapo alipo kajiweka.

Huu ni wakati wa Watanzania kujitambua na kuujua udhaifu wetu ulipo na kujua nguvu yetu iko wapi, ni lazima tuujue na kuukubali ukweli kwamba malalamiko na manug’uniko hajawahi kutatua tatizo lolote hapa duniani, kwa hiyo tunaweza kusema kulalamika na kunun’gunika kuwa wanyonge wa nchi hii bila kuchukua hatua ni unafiki na dhambi isiyostahili msamaha.

Ni muhimu kutambua kuwa uchaguzi au kura yetu ina maana kubwa sana, hiyo ndiyo elimu ya watoto wetu, kama una kero na kesi nyingi za ardhi mabazo hazina ufumbuzi, halamshauri yako unaishuhudia jinsi inavyonuka rushwa na jinsi wnaanchi mnavyookena kero na takataka unapokwenda kushughulikia suala lako la ardhi, iwe kupimiwa au kununua kiwanja, hapo utambue kuwa, hapo ujue hauna diwani.

Wala huhitaji kumlalamikia mtu tambua kwamba jicho lako ulilolipelekea kukumulikia ndani ya halamshauri yako na kusimamia watendaji wanaokunyanyasa kama mkimbizi ndani ya nchi yako, ama ni bovu au limepofuka kabisa, na jicho hilo haliwezi kuwa jingine isipokuwa diwani wako.

Huyo atakuwa ama hana uwezo wa kupambana na kuwasimamia vyema watendaji wabovu na wala rushwa au kaamua kujinga nao kwa kuwa ufisadi nchi hii kwa sasa ‘unalipa’ na wewe mwananchi unayefisadiwa unaona ndiyo ujanja, unaubariki na kuushabikia.

Hali inapanda ngazi hivyo hivyo kutoka kwenye halmsahauri mapka kwenye taifa, ukiona elimu ya nchi inazidi kuporomoka, waziri anajiendeshea wizara kama ka NGO kake, mitihani inaibwa barazani kama watoto wa darsa la pili wanavyoibiana kalamu za risasi na vifutio, halafu watendaji wakuu wanaendelea kutamalaki ndani ya mamlaka ya baraza la mitihani, hapo ujue kurunzi (mbunge) yako uliyoipeleka kwenye lile jumba la kifalme pale makao makuu ya kusadikika ya nchi, kuimurika serikali ikutumikie vyema ama imezima ahaina betri au imeribika ahitengenezeki, unatakiwa kuchukua hatua za haraka kufanya mabadiliko.

Wanafalsafa wanasema ‘Politics are too serious matters to be left to politicians alone’ kwamba siasa ni jambo nyeti na muhimu sana kuachwa wanasiasa peke yao . Kwa hiyo harakati za siasa zinazoendelea sasa kaika kila kona ya nchi, hata kama huhusishwi zinakuhusu sana , anza kuzifuatilia na ufikie uamuzi muafaka kujibu maswali yako ambayo huna hata wa kumuuliza.

Wakati mwingine utandawazi utusaidie kjifunza baadhi ya mambo mazuri, isiwe kuiga uvaaji wa nguo za ajbau na tabia zinazokinzana na uafrika wetu tu, tunaweza pia kuutumia vizuri.

Wananchi wa Massachusetts juzi wamemwonyesha Rais Obama gharama za kutotimiza ahadi zake kwa kipindi cha mwaka mmoja tu, sisi tunashundwa vipi kuwapa somo hilo hilo madiwani amabo wamekuwa wakituahidi kwa miak nenda rudi, tunashidnwa nini kuwaadabisha wabunge ambao wamegeuka kama nembo za majimbo yetu lakini hawana jipya, tunahindwa nini kutumia kipimo hicho hicho kumpima rais wetu kama kwa miaka hii mitano anayomalizia anatufaa kuendelea au la?

Uchaguzi ni kuchagua mustakabali wetu kama taifa, kila tunapompima mtu tumpime kwa vigezo vya hatma na majaliwa ya Tanzania , kutumia vigezo vya urafiki, mwenzetu au mazoea tu, ni kulinyesha sumu ya mamba taifa letu. Inawezekana tutimize wajibu wetu.

Mungu ibariki Tanzania , wabariki na watu wake wajitambue.

drbugaywa@yahoo.com 0754 449 421

Tuesday, December 22, 2009

Taifa halina nguo, nani atalivisha?

Na Deus Bugaywa

Bwana Yesu akiwa katika kilele cha mateso yake huku amelemewa na msalaba mzito, kuelekea Golgotha ambako alisuribiwa, akina mama wa Israel walikuwa wanabubujikwa machozi kumlilia kwa huruma ya mateso makali aliyokuwa akipata.
Lakini Mwenyewe aliwaambia kwamba hawana haja wala sababu ya kumlilia yeye, isipokuwa wajililie wao na nafsini zao n watesi wake kwa sababu ya dhambi zao na kwa kuwa upanga tayari uko juu yao.
Hatuwezi kubishana sasa hivi juu ya nchi yetu kuyumba, hilo ni jambo ambalo kila mwenye macho ya kuonana akili ya kufahamu analiona. Walau Kongamano la maadhimisho ya miaka kumi tangu kifo cha baba wa taifa limetufungua na kutambua kumbe mgogoro wetu uko wapi.
Na hivyo tunajua kwamba tangu mwaka 1995 nchi hii ingeweze kwenda segemnege kama inavyokwenda sasa kama isingekuwa kwa hekima na busara na kuogopwa na kuheshimiwa kinafiki kwa mwalimu Nyerere na wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM.
Nasema walimheshimu kinafiki kwa sababu walilazimika tu kukubaliana naye siyo kwa sababu walielewa na kuona mantiki ya hoja zake, lakini kwa kuwa walikuwa wanajua hawawezi kumudu kutofautiana na mzee huyo.
Kwa hiyo wakati dunia inaomboleza kifo cha mwana shujaa huyu wa Afrika wapo wanafiki wakubwa miongoni mwetu ambao walishusha pumzi za ahueni, kuashiria kikwazo kikubwa kilichokuwa mbele ya kufikia malengo yao ya ubinafsi na kuifanya Tanzania kama mali yao sasa hakipo tena. Na hiyo ndiyo hali tunayoiona sasa, hakuna mtu anaweza kumkemea mtu kufanya lolote lile kwa sababu zozote zile, taifa linakwenda kiholelaholela tu.
Pengine baada ya miaka kumi ya Tanzania bila baba wa Taifa tuna hoja za kujiuliza kama tunapaswa tuendelee tu kumlilia na kutamani kama angekuwa bado yuko hai kitu hiki au kile kisingefanyika au tuanze kujililia sisi wenyewe na nafsi zetu na kwa kweli kuchukua hatua za kuyaishi yale ambayo tunaamini kwamba ndiyo ulikuwa msingi wa Tanzania moja yenye haki na usawa?
Ni kweli kwamba sasa hivi katika CCM hayupo mtu anayeweza kuuliza maswali matatu, kama ambayo Mzee Butiku ametueleza, yale aliyoyauliza Mwalimu wakati wa mkutano Mkuu ule wa mwaka 1995.
Nani atawauliza viongozi wetu wa leo kama wao ni wahuni au viongozi? Na pili, kwa zogo na vurugu zile ndiyo staili ya kuchagua Rais? Na hili la tatu ndio la muhimu sana kwetu kwamba, Je Watanzania kama wangewaona, je wangeamini kuwa ninyi ni viongozi wao?
Walau jambo moja linajidhihirisha kwetu hapa ni kwamba wajumbe wanaokutana katika mkutano wa kuchagua mtu ambaye anatarajiwa kuwa Rais wa nchi hii, huwa wana mabo ya jabu ambayo Mwalimu hakusita kuwahoji tofauti ya mkusanyiko huo wa kuchagua rais na wahuni, hata yeye alifika mahali kashindwa kutambua hawa waliokutana humo ni viongozi au wahuni? Sina hakika walijibu nini.
Watanzania walau sasa tumeshaona na tunajua madudu mengi na jinsi viongozi wetu wanavyofanya, hivi bado tunaamini kuwa hao ni viongozi wetu? Mwalimu aliwashangaa na viongozi wale kwa kuwa alijua salama yao mbele ya Watanzania ni kwa vile walikuwa hajaona wanavyofanya mambo ambayo unaweza kuyaita ya kitoto wakati wana dhamana ya kuongoza nchi, na akajua laiti Watanzania wakijua bila shaka hawa wasingestahili kuwa viongozi, kwa sababu Watanzania wasingeamini kuwa hao ni viongozi wao.
Lakini ndio tulio nao, na ndio hao tunawashuhudia wakipashana na kuvuana nguo hadharani kweupe, kwenye majukwaa rasmi na kulumbana kwa maslahi yao binafsi kuliko ya kwa ajili ya mustakabali wa taifa, bado tunaamini hawa ni viongozi wetu?
Bila shaka ili kuisaidia nchi hii ni lazima kama hayupo mtu ambaye anaweza kuwauliza maswali hayo na wakamsikiliza na kumheshimu hata kama ni kwa unafiki tu, jukumu hilo linatuanguakia sisi wananchi moja kwa moja.
Kwa sababu hatimaye sisi ndio tunaolipa kila gharama ya madudu haya yanayofanywa na viongozi ambao wanajiita wanatokana na sisi hata kama wanayofanya na kutenda hayana maslahi kwetu kama taifa.
Ni lazima tufike mahali tuache kunung’unika na kulaumu kwa chini chini, tuchukue hatua za kuacha unafiki ili tuweze kulikoa taifa letu na hatari kubwa inayolikabili mbele yake kama tukiendelea na unafiki huu tunaokwenda nao kwa sasa.
Hata makada wa chama wanaojiita kwamba wako upande wa wananchi waoneshe hivyo kweli siyo kwa mashaka mashaka, kama kweli wameamua kupambana kwa ajili ya wananchi na kwa maslahi ya Tanzania hawana haja kung’ang’ania kujinasabisha na watu ambao wanaamini kuwa wako kinyume chao.
Giza na nuru haviwezi kukaa pamoja hata kwa bahati mbaya, kimoja kikiwepo lazima kingine kikimbie, kama kwa mfano ndani ya CCM wako watu ambao wanatuhumiwa ni mafisadi na ambao ndiyo wanaiyumbisha nchi hii, na kuna wengine ambao wanaamini ni wasafi, hakuna namna hawa wanaweza kukaa pamoja, mwanga hata uwe hafifu namna gani ukiumulika kwenye giza utajipambanua tu.
Tunaambiwa Mwalimu katika mkutano mkuu ule aliwambia wajumbe kama wataendelea na msimamo wao wa utovu wa nidhamu na kushabikia mgombea aliyewahonga, basi waende kwa wananchi, wao wapite huku na wengine wapite kule waone wananchi wataamua nini.
Kama CCM inahitaji kuendelea kuwepo apatikane mtu wa aina hiyo, lakini bahati mbaya kubwa kwao ni kwamba hawana mtu wa aina hiyo, kila anayetaka kuwaeleza na kuwasaidia wauone ukweli wanakurupuka na visingizio vya kitoto kwamba anayesema anatafuta umaarufu au ana wivu kwa kuwa alishindwa katika uchaguzi au hakuwa mwanamtandao.
Ndio maana nasema kutokuwepo kwa nabii au mtume hakuna maana kwamba mafundisho yake hayapo, kawaida manabii wanakuja na kuacha ujumbe ambao unatarajiwa uwaongoze wafuasi kwa muda wote ambao nabii hatakuwepo.
Ni kweli baba wa taifa hatuko nae lakini sisi ambao tunaamini hekima zake zina umuhimu wa pekee kwa ajili ya kuijenga Tanzania yenye amani na usawa hatuna hiari ila kuvaa viatu vyake na kuanza kuisimamia misimamo yake.
Tumeambiwa nchi inatembea uchi, na ni kweli ukiangalia unaona kabisa hakuna hata rapa la nguo la kuistili, watu pekee wenye kumudu kuistili ni sisi ambao tunaona na kukubali ukweli kwamba taifa liko utupu.
Hatuwezi kuwategemea wale waliolivua nguo taifa hili walivishe, kwa sababu hawafanyi hivyo kwa bahati mbaya, wanalivua nguo taifa makusudi kwa malengo maalum, na siyo kwamba hawajui kuwa liko utupu la hasha, tofauti yetu na wao ni kwamba wakati sisi tunakiri hivyo wao hawataki kukiri ukweli huo.
Ni wajibu wetu bila kujali itikadi zetu, wajibu huu unatuangukia sisi kama Watanzania siyo kwa sababu nyingine yeyote ile, na kwa hili hakuna mwenye hisa zaidi ya mwingine, hatujachelewa kiasi hicho kama tukimua sasa kuuvua unafiki bado tuna muda tunaweza kulikoa taifa hili.
Mungu ibariki Tanzania.
0754 449 421, drbugaywa@yahoo.com

Friday, October 30, 2009

He’s my brother reviewed

Deus Bugaywa

Binyavanga Wainaina’s He’s my bother story is very interesting, especially if you are a novelist like I am, it will be even more interesting if you are an east African.

It tells about African Hospitality in attending guests, in a Tanzanian way. The author tells his audience how Tanzanians are still maintaining the natural African generosity, that they perceive all people are equal and relative to one another.

He is telling us that for Tanzanians hospitality is exceptional that it can hardly be found anywhere in the continent especially in these era where all Africans are moving violently the Western way.

“In which other African airport can you get real assistance? I walk from one official to another, irate that my luggage seems to have disappeared. Everyone is hugely supportive and soon the entire airport seems to know that my luggage is missing and I am headed for a funeral. I am overwhelmed by assistance.” He narates.

In all he is trying to send the massage that Tanzania is one of the very few country that still maintains the African communal values of hospitality unlike her colleagues who “like to feel that we are a progressive people who have left all this communal African nonsense and acquired a hard-nosed get-with-the-programme attitude.”

In my opinion the author has done a god job to explain the true nature of Tanzanian, especially on the issue of Tribalism, as the experience he get at the open air traders space they went for dinner. Its true that in Tanzanians daily life no body bothers to ask a colleague his or her tribe, even if they meet for the first time.

Wainaina is Kenyan author born in Nakuru, get his early eduactaion in Kenya before going for further studies in Souther Africa at Transkei University. After his Study he nmoved to Cape Town where he is living and working as writer on tourism issues.

In 2002 he won the Caine Award for African literature, he is the founder of the Kwani magazine. He is now working on his novel The fallen World of Appearance.

Thursday, October 29, 2009

The fourth day rolls on



Wadau wa mafunzo ya mtandao wakiendeleza shule ya mambo ya mawasiliano ya kisasa katika ukumbi wa chuo cha Benki Kuu Mwanza

Deus Bugaywa

Had it been a soccer match, one could easily say the internet workshop for media personnel and stakeholders in Lake Zone has reached a semi - final stage, as the fourth day proved to more interesting just as a real semi - final of archrivals could be.

The trainer Peik Johansson started the session by introducing the class to famous world news agencies and how to reach and use them as journalists. The Inter Press Services (IPS) news agency caught the interest of many as it happened to be different from the rest of the news agencies.

It was learned by the participants, through the facilitator, that unlike many big news agencies, the IPS uses local journalists to report what is happening in their locality which has the international touch.

This interested some of the participants to join the agencies as correspondents; it was luck for them that, Mark Gideon of Misa - Tan, promised to provide them with IPS form for those interested by being IPS stringer.

Linking the sources from ones blog was the subject that followed; participants were able to link the sources of what they put on their blog to make it easy for the readers to follow the origin source.

After the linking session, we arrived at the core of the training, the Journalistic research via internet, here journalists were taken back to there earlier years in journalism class, where they were reminded to always keep in mind the famous 5Ws (and the H of course), the who, what, when, where and why, while making internet searching.

As it should be expected from any best trainer, after an interesting and fruitful lecture, participants were give a home work, to use their internet searching skill by using international and local sources to write a short notes, explain or describe (depending on the need of a specific question) the Childhood of US president, albinos situation in Tanzania na the court cases, the Nesttle Boycott, the WTC Building 7, climate change and effects to Mt. Kilimanjaro and give opinion on Wainaina’s short story “He si my brother” .

The final will be tomorrow where the training will be brought to a close, where participants will be equip with the skill of how to upload pictures to their bolgs.

Wednesday, October 28, 2009

The workshop continues

The workshop continues
Deus Bugaywa
The internet workshop for lake zone communicators has continued for the third day today where secrets of the modern world means of communication keeps unfolding to the participants.

After the review of the previous day session participants, the today’s session started by visiting different media web sites in order to provide trainees with the knowledge on how to open web sites in search of information and other materials of their interest.

This was followed by the e mailing skills whereby trainee were equipped with the skills on how to use the internet as a perfect tool for communication both leisure and official, some of the official and friendly e mail were displayed to enable the class undersdtand the subject well.

The class was able to go through some websites which offer useful e - mail rules, some of these sites are http://email.about.com and www.systemarchitecture.org which, member of the class find them very useful.

Other interesting topic for the third day session was the plagiarism where the class was asked to visit the Copyright and neighboring rights act of 1999 at to learn more about plagiarism and copyrights.

In the evening session the class had the assignments of how to get specific information on the web sites, the subject which was very interesting. Though some of the searching proved to be a bit difficult to go through.

The trainer warned the class not to immediately trust any website instead they have to to reliable ones and see to it that they get the information from the original source.

The training is proving to be very useful for the participants as Calvin Jilala put it on the “We found that internet has brought about a multiplied number of information potential sources. Mr Peik took us through global source of news, whereby he explained about how to search for facts or background, search for the people and facts editing, security copy and grammar-remote access (even if your soft copy tool has misbehaved you can always go back to the copy in an e-mail to recover it)”.

The training is expected to continue on the forth day tomorrow before it come to an end on Friday where one of the Tanzania’s famous blogger, Majid Mjengwa will join Mr. Johansson as a guest trainer.

Tuesday, October 27, 2009

the second day

By Deus Bugaywa

The Internet Training for Lake Zone Journalists has entered its second day whereby trainees are tremendously gaining pace in the use of the technology that has changed the world.
The training which is organized by MISA Tanzania chapter in collaboration with the Finnish Foundation for Media and Communication and Development (VIKES) has been a major stepping stone towards modern journalism for many press men and women in the lake zone.
The second day has seen all participant taken through the main world web that has changed the world, they learned on how to e shopping works, maps, information and image searching has been made easier by the new technology.
Apart from familiarizing with the most popular world wide websites, the trainer Peik Johansson demonstrated for the class on how to create a blog, the subject which was of interest to almost all participants.
At the end of the blog making lesson all participant were able to make their own blog, it was a dream come true to many journalists in zone where very few of them were blog visitors let alone having their own.
Of the very interesting webs was the you tube, where a video clip of street footballer captured the attention of many in the class, the other interesting site was the Wikipedia where they were able to adit some Swahili worlds in the web.
However Mr. Johansson warned the trainee not to trust all is seen in the web until they confirm them on the original sources.
“To me this is a very big achievement because even if we have not yet completed the the tarinning I feel more confident to search for information as much as possible” observed George Ramadhan one of the participant who is very impressed with the training.

Karibu 2009

Karibu 2009!

Na Deus Bugaywa

Kila siku ni siku mpya, wahenga walisema, kwamba kwa mtu makini mwenye kujifunza kutokana na uzoefu na mwenye kutazama mbele leo ni siku tofauti kabisa na jana, hii ni siku nyingine inayokuja na changamoto zake. Hekima hii hata hivyo haimaanishi kwamba hakuna cha kujifunza kutokana na siku iliyokwisha.
Ni kutokana na kujifunza kutokana na makosa au mapungufu yaliyotangulia ndio maana siku inayoanza inakuwa ni mpya kwa maana kwamba yako makosa yaliyofanyika na mapungufu yalioonekana kwa hayo yakitumiwa vyema yanawez saidia leo kuondokana na makosa yale yale yaliyofanyika jana.
Kama taifa tunaanza mwaka mpya, ambao nina imani utakuwa wa kheri na neema kwa Tanzania kama tu tukijifunza kufuata kanuni ya historia kwamba ili tujue tulipo ni lazima tutazame tunakotoka, na ili tufahamu tuendeko ni muhimu sana kutazama tulikotoka na mahali tulipo sasa.
Mwaka huu utakuwa mpya kwa maana ya kuutofautisha na uliomalizika kama tu tutakubali kujifunza kutoka mwaka 2008. Mwaka wa jana umekuwa na mengi ya kujivunia lakini pia umekuwa na changamoto zake nyingi tu ambazo kama tukiamua kwa dhati, tunaweza kulikomboa taifa letu kutoka katika minyororo ya umaskini, ujinga na maradhi.
Mwaka jana umekuwa ni mwaka wa aina yake katika historia ya nchi hii, umeshuhudia kwa mara ya kwanza kuvunjwa kwa baraza la mwaziri kutokana na waziri Mkuu wa kujiuzulu kwa kashfa ya Richmond .
Katika hili liko somo moja muhimu sana kwetu kama taifa kwamba tunachokikosa hasa katika kutekeleza majukumu yetu mbali mbali ni dhamira ya dhati ya na uzalendo.
Hakuna ubishi kwamba kazi iliyofanya na kamati ya Mwakyembe na wenzake ni kielelezo na kipimo cha kujitoa kwa hali ya juu kwa kutetea hadhi na heshima ya Tanzania na Watanzania. Yako mambo mengi yanashindwa kufanyika kwa ukamilifu au hata hayafanyikki kabisa kwa sababu ya watu kutokuwa na moyo wa uzalendo kwa nchi yao .
Tumekuwa taifa la watu wa ajabu, ubinafsi umekuwa ndio mfumo wa kupigania maisha yetu, wako baadhi yetu, na ni wengi kweli, ambao hata kama akitakiwa kutimiza wajibu wake wa kawaida kabisa na anaolipwa kwa ajili hiyo hawezi mpaka kwanza ahakikishiwe kunufaika na kile anachotakiwa kukifanya.
Matokeo yake kila mtu sasa anapigana vita yake mwenyewe ili kuweza kuyafanya maisha yaende, hakuna mtu anakumbuka kwamba liko taifa ambamo ndio tunaishi na kwa vile hatuna nchini kwetu kwingine ni lazima tuhakikishe nchi yetu inakuwa salama katika hali zote.
Hakuna mtu siku hizi anahagaika na maslahi ya taifa hili, kila mtu anakufa na lwake kuhangaikia maslahi ya familia yake na vitegemezi vyake. Bahati mbaya sana ni kwamba harakati hizo za kujinufaisha binafsi zinafanyika kwa gharama ya kulibungua taifa.
Ziko dalili za wazi kabisa kwamba taifa hili sasa linajijenga taratibu lakini kwa uhakika kuwa tifa la matabaka. Hali hii nayo hakuna mtu anahangaika nayo watu wako ‘bize’ wakipigania maisha, hakuna anayekukosa usingizi kwa ajili ya mustakabali wa taifa hili.
Ubinafsi huu sasa umetufikisha katika hatua ambayo unaweza hata kusikia kinyaa kujiita binadamu. Ili kudhihirisha taifa hili na watu wake sasa wamejichoka na kushindwa kuheshimiana na kuthaminiana, tumefika hatua mbaya sana ya kipuuzi na kwa hakika ni ya kishenzi.
Kwamba sasa tumekosa ubinadamu kwa kiwango kisichoelezeka hata kufikia hatua ya kuona viungo vya binadamu mwenzako ni bidhaa ambayo unaweza kubadilishana kwa ajili ya kupata utajiri, huu ni ujuha na wendawazimu uliopindukia mipaka.
Haya yanatokea katikati ya jamii yetu na wako wanajamii ambao wanawajua kabisa wahusika lakini kwa sababu zinazojulikana na wao wenyewe tu, hawataki kujitoa kuwataja wahusika kwa ajili kulinusuru taifa hili na balaa hilo .
Kwa hiyo kama kuna somo moja tunalotakiwa tuiingie nalo kwa ajili ya utekelezaji wa maazimio ya mwaka 2009 ni kuanza kujenga uzalendo kwa ajili ya ustawi wa taifa letu. Ni lazima tutambue na kuukubali ukweli kwamba bila moyo wa kujitoa na hata wakati mwingine kuumia kwa ajili ya wengine hatuwezi kabisa kuufikia ukombozi wa taifa hili tunaoupigania.
Na kujitolea huku kunamhusu kila mwana wa taifa hili, kila anayeitwa Mtanzania na mwenye mapenzi mema na nchi hii ni lazima kwa hakika tuache kelele za kusubiri matatizo yatokee ndio tuanze kutafuta mchawi wakati mambo yalishaharibika.
Hakuna kitu kizuri ambacho unaweza kukipata ukiwa tu umetulia mahali au unasubiri wengine wakuletee, ni lazima tukubali kutimiza wajibu wetu kikamilifu. Tuaachane na utepetevu wa akili kudhani kwamba wako watu mahali fulani watakuja kutusaidia. Jinsi tunavyotaka nchi yetu iwe ni azima sisi wenyewe tuwajibike kuifaya iwe hivyo.
Rushwa na ufisadi uliotapakaa nchi hii msingi wake uko katika ubinafsi, mtumishi wa umma anafika mahali anasahau kwamba cheo hicho ni dhamana kwa hiyo anapaswa kufanya kazi manufaa ya aliyempatia dhamana hiyo.
Mwaka jana pia umetusaidia kutambua wawakilishi wetu ni watu wa aina gani, wabunge wetu ni watu muhimu na wadau wakubwa wa maendeleo ya taifa letu hasa kwa jukumu lao la kuithibiti serikali katika matumizi yake.
Uzoefu wa bunge la mwaka jana umetuonesha kwamba wakati tunaingia katika uchaguzi wa wabunge na wawakilishi wengine, yaani madiwani ni muhimu sana kuangalia aina ya mtu tunayemchagua kuliko chama. Tumeon jinsi baadhi ya wawakilishi wetu wanavyogeuka kuwa wasemaji wa serikali na wawakilishi wa vyama badala ya kuwawakilisha Watanzania wa majimbo yao .
Chama kinaweza kuwa kina sera nzuri na nzito sana za kimaendeleo lakini zikaishia katika kutamkwa tu kwenye mikutano ya kuomba kura, halafu mtu anayepewa jukumu la kuhakikisha sera hizo zinatekelezeka anakuwa hana uwezo huo.
Hili limejidhihirisha kwa uchache wa wabunge wa upinzani bungeni na baadhi ya wachache toka chama tawala, yako mambo ambayo katika hatua zake za awali yalionekna kama mchezo tu wa kuigiza kwa kupuuzwa na hata kukejeliwa na baadhi ya wawakilishi wetu lakini ambayo sasa yamegeuka kuwa masuala makubwa yenye uzito mkubwa kwa mustakabali wa nchi hii.
Kwa hiyo tunapomshukuru Mungu kutujalia kuuanza mwaka 2009 salama, tudhamirie basi kuhakikisha kwamba tunajitahid kila mmoja wetu kuweka mchago wetu chanya katika ujenzi wa Tanzania mpya ambayo kila mmoja wetu anaiotea ndoto.
Siyo bahati mbaya kwamba mimi na wewe tumebaki kuingia mwaka huu, wataalamu wa teolojia wanatuambia kwamba Mungu na makusudi maalum na kila mtu aliyemuumba, pengine kusudi lake kwako wewe Mtanzania uliyejaliwa kuwa hai mpaka wakati huu ni kuleta mabadiliko katika taifa hili.
Hakuna kinachoweza kushindikana kama tukiamua kwa dhati, kama mwaka jana tulishindwa hatuna sababu ya kulalamikia yaliyopita, kwani hayo si ndwele, sasa tugange yajayo. Na kwa kuwa kila siku ni siku mpya na hivyo mwaka huu ni mwingine tofauti na wa jana basi tuamue uwe mwaka wa ukombozi wetu katika kila uga wa jamii yetu, uwezo wa kusababisha mabadiliko tunao, kinachotakiwa ni kudhamiria tu.
Mungu ibariki Tanzania .
drbugaywa@yahoo.com 0734 449 421