Friday, February 5, 2010

CCM, mchelea mwana kulia…!

Na Deus Bugaywa



Chama Cha Mapinduzi leo kinatimiza miaka 33 tangu kuzaliwa kwake tarehe 5, Februari, 1977 baada ya kuungana kwa vya vya TANU na ASP na kuunda chama kimoja kilichoitwa cha Mapinduzi.

Kiliunda cham kipya kikiwa ni mrithi wa wazazi wake waliokitangulia ambao kwa namna moja ama nyingine walihusika na ukombozi wa Tanzania na kutuwezesha kupata uhuru toka wa Mkoloni na Usultani wa kiarabu kwa Zanzibar.

Hiki ni chama ambacho kiliundwa kwa makusudi maalum ya kuwatetea wakulima na wafanyakazi wa Tanzania , kilikuwa na malengo mahsusi ya kumkomboa mwananchi mnyinge kutoka katika unyonge wake na kumfanya mtu anayetahamniwa.

Kwa sababu madhumuni ya kupigania uhuru hayakuwa kumwondoa tu mkoloni wa kizungu ndio unyonge wa mwafrika wa Kitanzania utakuwa umekwisha, ndio maana kikaundwa chama hiki ili kumwezesha mwananchi huyo kupata na kuweza kuiishi tafsiri na maana halisi ya kuwa uhuru.

Kwa maana nyingine CCM kiliundwa ili kiweze kumwzesha Mtanzania kujikinga na wimbi la wanyonyaji na walanguzi wa wakati huo ambao waliona na kamiani kwamba mafanikio yao hayawezi kuja bila kuwafanya watu wengine kuwa dhalili.

Kwa hiyo siyo bahati mbaya kwamba moja ya misingi iliyokiundiwa chama hiki iliyolithiwa toka TANU ni msingi wake wa kwanza unaowataka wanachama wake kuamini kwa dhati kwamba binadmau wote ni sawa na ndugu zangu na Afrika ni moja.

Tena ikasisitizwa kwamba pale mtu anapopewa heshima ya kuwangoza au kuwatumikia Watanzania wenzake asijione kuwa ndiyo amekuwa ‘mkoloni mweusi’ wa kuwanyasa wenzake au kutumia mali ya umma kama vile ni mali yake binafsi.

Hawa wakakukbushwa kuwa cheo ni dhamana na wakatakiwa kutotumia vyeo hivyo kwa manufaa yao binfasi isipokuwa kwa ajili ya utumishi na maslahi ya umma na ni umma tu ndio unaotakiwa ufaidike na utumishi wa mtumishi huyu wa umma na vinginevyo.

Bila shaka tutkubaliana kwamba msingi mwingine muhimu katika ukuaji na hatimaye kufikiwa malengo ya taasisi au chama chochote kile ni ukweli, kwa maana na tasira zake zote, wana CCM hapa walisisitizwa kusema kweli daima na fitina kwao iwe mwiko.

Hii na Minsingi mingine imekifanya chama hiki leo kufikia umri huu na kukifanya moja vyama vikongwe kabisa vya siasa sio tu katika Tanzania lakini pia ndani ya bara la Afrika.

Bila shaka wana CCM wanahitaji pongezi hili, kufikia umri huu ni kazi kubwa mabyo siyo vyama vingi vyenye lika moja an CCM vimeweza kufikisha umri huo vikiwa bado ni vyama tawala. Kwa hili tu wanastahili pongezi hata kama namna ya kufikisha kwao umri huu kunahitaji mjadala lakini walau wafika.

Pamoja na pongezi hizo, hata hivyo, ni jambo jema pia kwa wenye chama chao hiki, kuongozwa na hekima ya kawaida kabisa katika maisha haya kwamba, kitu cha muhimu katika maisha haya siku zote siyo pale ulipo isipokuwa ni wapi nuanelekea.

Mtu yeyote makini habweteki na kufika pale alipofika, isipokuwa anakaza mwendo kuweza kuongeza nguvu na kurekebishwa mwelekeo wake ili asiende kombo. Atatumia uzoefu, kwa kutahimini uwezo na mapungufu aliyokuwa nayo katika kufika hapo alipofika.

Ndio maana ni muhimu kwa wanachama wa chama hiki wanapofurahia siku ya kuazaliwa kwa chama chao, wajiulize swali wana umbali gani wa kwenda wakiwa katika furaha hii ya sasa?

Watakubaliana na mi kwamba wamefika hapa kutokana na misingi imara iliyosimamiwa na uongozi thabiti wa chama hicho, ambao sina hakika sana kama wanaweza wakasimama kifua mbele wakasema wanao uongozi wa aina hiyo ndani ya chama chao kwa sasa unaweza hata kushabihiana kwa nusu wa ule uliowaasisi na kuwawezesha kuweza kusafiri safari hii ndefu mpaka hapa walipo leo.

Wenyewe ni mashahidi wa jinsi ambavyo mpaka hapa walipofika bado wanasafiria kivuli cha utahbiti wa viongozi waasisi wao hata baada ya miongo miwili kupita tangu kiazi chao kipya kiakbiziwe chama.

Alichofanikiwa kwa kiasi kikubwa ni kuivunja vunja miiko hiyo n badala yake sasa chama kimekosa ile maana yake halisi ya kuwa kundi la watu wenye dhamira na nia moja katika kutekeleza malengo yanayofanana.

Leo katika CCM wapo wanachama mahiri wengi tu lakini, kama si mnafiki huwezi kukiita chama hicho ni kimoja kwa hali ilivyo sasa. Ni kundi moja ambalo lakini kila mwana kikundi anasababu zake tofauti kabisa na mwenzake za kuwemo ndai ya kundi hilo na namna tofauti kabisa tena zinazokinzana za kueteleza malengo hayo.

Ni kama timu inayoundwa na wachezaji wazurina mahili wa kimataifa lakini ambao hawana ushirikiano wa kitimu ‘team work’. Kila mchezaji anakuwepo pale isyo kwa ajili ya kufunga magoli lakini kwa ajili ya kuonyesha jinsi alivyo mtaalam kulamba chenga maadui zake, na kuwaonyesha maadui zake (wa ndani na nje ya timu) namna anavyoweza kumudu mpira, lakini ujuzi huo haumsaidii kufunga magoli.

Ndiyo umvyoweza kuiliezea CCM ya sasa, ambayo pamoja na kusherekea umri huo uliotukuka ukilinganisha na vyama vingine vya siasa nchini, kwa hakika badao kinaoneka kana kilizaliwa baada ya mfumo wa vyama vingi, na kwamba labda ndio kinajifunza siasa. Ukikitazama kwa makini kwa kweli huwezi ukaona umri wake unaakisiwa katika namna kinavyojiedesha.

Kwanini kimefika hapa, bila shaka ni kutokana na kutosikia la mkuu na hivyo kinajikuta taratibu na kwa uhakika kinapoteza miguu. Wahenga wetu wamewahi kutuonya kuwa ‘Mchelea Mwana kulia, hulia yeye’.

Kwamba ukiwa wewe ni mlezi wa mtoto halafu anapofanya kosa hutaki kumkanya kwa vile unaogopa atalia basi wewe ndiyo ujiandae kulia. Na hiki ndicho kilichoikuta CCM.

Kumekuwa na ungonjwa mbaya kabisa usiofaa wa kulindana ndani ya chama hiki, mtu akifanya kosa ambalo kwa tartaibu za kawaida tu ama anatakiwa awajibike au kama si muungwana anakuwa na kiburi hataki kuwajibika basi awajibishwe na mamlaka anayowajibika kwayo.

Hili limekuwa haliwezekani ndani ya chama, kiemfika mahali kinadhani kwamba ni chenyewe tu chenye hati miliki ya kutawala nchi hii, na zaizi sana kinadhani Watanzania wote ni wajinga kiasi kwamba wanaweza kuafanya madudu yao halafu wakaendelea kuaminika tu na wananchi kwa kiwango kile kile, hili ni kosa moja kubwa wanalofanya CCM.

Kiongozi wa chama anapokosea au anapopatikana na kashfa ambazo zinaweza kuharibu sifa na jina la chama kwa wananchi utasikia viongozi wa cham tena wengine wa kitaifa eti wakikitetea chama kwamba huyu aliyefanya hivyo mwanachama wa CCM siyo CCM.

Halafu mtu huyu hata hawajiishwi walau kisiasa ili kweli chama kiwezi kujitenga nae na wananchi wajue kweli kwamba kimejitenga na mkosaji au mtuhumiwa huyo, lakini kuendelea kumkana mtuhumiwa halafu upande wa pili kinaendelea kumkumbatia, huko ni kujiandalia mauti.

Ni vyema, kama inataka kuendelea kuishi, CCM ikajifunza kwa wazee wenzake Kenya , Zambia , Malawi ili irekebishe makosa yake. Kila lakheri CCM katika umri huu

drbugaywa@yahoo.com 0754 449 421

No comments:

Post a Comment